Home » » BIKIRA MARIA KATIKA WOKOVU WETU

BIKIRA MARIA KATIKA WOKOVU WETU




 
MATANDA RICHARD- MWANAMARIA
DHIMA YA BIKIRA MARIA KATIKA MPANGO WA WOKOVU INAONESHWA WAZIWAZI KATIKA MAANDIKO MATAKATIFU.
Maandiko Matakatifu ya Agano la Kale naya Jipya na Mapokeo ya  kale yaonyesha wazi zaidi na zaidi dhima(KAZI) ya Mama wa Mwokozi katika mpango wa wokovu, na kuiweka mbele yetu tuifikirie. Vitabu vya Agano la Kale vyaeleza historia ya wokovu ambavyo ndani yake hutayarishwa polepole ujio wa Kristo ulimwenguni. Maandiko hayo ya Kale, yanavyosomwa katika Kanisa na kufahamika katika mwanga wa ufunuo kamili wa baadaye, hatua kwa hatua yabainisha zaidi na zaidi sura ya yule mwanamke aliye Mama wa Mkombozi. Katika mwanga huu anabashiriwa kinabii katika ahadi ya ushindi juu ya nyoka waliyopewa wazazi wa kwanza baada yakutenda dhambi (taz. Mwa 3:13).

Vilevile yeye ni Bikira yule atakayepata mimba na kumzaa Mtoto mwanamume ambaye jina lake ataitwa Emanuel CHUKUA BIBLIA YAKO  UFUNGUE KITABU CHA NABII Isa 7:14; Mik 5: 2-3; Mt. 1:22-23). Yeye anashika nafasi ya kwanza miongoni mwa wanyenyekevu na maskini wa

Bwana,ambao, kwa matumaini ya imani wanangojea na wanapata wokovu kwake. Hatimaye kwa yeye, Binti mtukufu wa Sayuni aliye bora sana, baada ya kungojea kwa ahadi kwa muda mrefu, nyakati zilitimia na mpango mpya wa wokovu ukawekwa, hapo Mwana wa Mungu alipotwaa maumbile ya kibinadamu kutoka kwake, ili amkomboe mwanadamu katika dhambi kwa mafumbo ya mwili wake.

 Mungu wa huruma alitaka Umwilisho utanguliwe na ukubali wake yeye aliyeteuliwa tangu milele awe Mama, ili kama vile mwanamke alivyoshiriki kuileta mauti, kadhalika mwanamke asaidie kuuleta uzima. Hayo yamhusu kwa namna ya pekee Mama wa Yesu  aliyeuzalia ulimwengu Uzima wenyewe, utengenezao yote upya, naye alitajirishwa na Mungu kwa karama zenye kustahili jukumu hili kubwa hivi.  Kwa hiyo hatuwezi kushangaa ikiwa Mababa Watakatifu walizoea kumwita Mama wa Mungu kuwa  “ Mtakatifu kabisa”,  bila doa lolote la dhambi kama alivyotengenezwa  na Roho Mtakatifu na kufanywa kuwa kiumbe kipya (176)  Hali amepambwa tangu nukta ya kwanza ya kutungwa kwake mimba kwa kwa mng’aro wa utakatifu wa pekee kabisa, Bikira huyu wa Nazareti aliamkiwa na  Malaika mhubiri (Angelo nuntiante),  Kwa amri ya Mungu kuwa “ Mtakatifu kabisa” kwa amri ya Mungu, kuwa “amejaa  neema”(Gratia plena)
Soma injili ya.Lk 1:28 naye akamjibu mjumbe huyu wa mbinguni  “Tazama mimi ni mjakazi wa Bwana na iwe kwangu kama ulivyosema” (Lk 1;38). Hivyo Maria, binti Adamu, kwa  kulikubali Neno la Mungu amekuwa  mama waYesu, na akiyakumbatia kwa  roho yake yote, na bila kushikwa na dhambi yoyote, mapenzi ya Mungu yenye wokovu, akajitoa kabisa kama mjakazi wa Bwana kwa ajili ya nafsi ya Mwanawe na kwa kazi yake, akilihudumia fumbo  la ukombozi chini yake na pamoja naye kwa neema ya Mungu Mwenyezi. Kwa hiyo Mababa Watukufu huona kwa haki kuwa Maria hakutumiwa na Mungu katika hali ya kutendwa tu, bali alishiriki kuleta wokovu wa binadamu kwa imani yake na utii wake wa hiari.
Mt. Irenesus anasema, yeye , “kwa kutii amekuwa sababu ya wokovu, kwa ajili ya kizazi chote cha wanadamu” hili ni jambo la fur asana kwetu sisi wana wa mama yetu na tunajivunia kwa kuwa na Maria kama mama yetu na Yesu kama kaka yetu anayetupenda.
Ndiyo sababu, Mababu wa Kanisa wasio wachache hupenda kueleza katika mahubiri yao kwamba “Fundo la kutotii kwa Hawa(EVA) limefunguliwa kwa utii wa Maria; na kile ambacho Hawa  alifunga kwa kutosadiki kwake, Bikira Maria alikifungua kwa imani yake”(178).Wakimfananisha [ Maria] Hawa, wanamwita Maria “Mama wa walio hai na mara nyingi wanakitangaza  maneno   “Mauti yalikuja ulimwenguni kwa njia ya Hawa na  uzima umeingia ulimwenguni kwa njia ya Maria ”
 Umoja huu wa Maria na Mwanawe katika kazi ya wokovu unaonekana tangu dakika  ile Bikira alipotunga mimba ya Kristo mpaka kifo chake. Kwanza Maria alipoondoka kwenda kwa haraka kumwamkia Elisabeti  akasalimiwa naye kuwa mwenye heri kwa imani yake katika wokovu ulioahidiwa, na mtangulizi akaruka ndani ya tumbo la mama yake fungua Biblia yako injili ya Luka Lk 1: 41-45 tena,  wakati wa kuzaa, Mama wa Mungu alipowaonyesha wachungaji na mamajuzi kwa furaha Mwana wake mzaliwa wa kwanza asiyepunguza ukamilifu wa ubikira wake bali akautakatifuza (181) Na alipomtolea  Bwana hekaluni, pamoja na sadaka ya maskini alimsikia Simeoni akiagua kwamba Mwanae atakuwa ishara itakayonenewa,  na kwamba upanga utaingia moyoni mwake mama ili yafunuliwe mawazo ya mioyo mingi ( taz Lk 2:34-35)
Walipomkosa mtoto Yesu na kumtafuta kwa huzuni wazazi wake wakamwona hekaluni akiyashughulikia yale yaliyo ya Baba yake, wala hawakuelewa neno hilo  la Mwana. Lakini mama yake aliyaweka   haya  yote   moyoni  mwake akitafakari, fungua injili ya Lk   2:41-51)
Maria katika maisha ya hadharani ya Yesu
Katika  maisha ya hadharani ya Yesu, mama yake alijionyesha tangu mwanzo kwa njia ya pekee katika arusi ya Kana   ya Galilaya aliposababisha kwa huruma yake chanzo cha ishara za Yesu aliye Masiya, kwa njia ya maombezi yake, (taz Yn 2: 1-11). Wakati wa kuhubiri kwake Mwanae alipokea maneno ambayo kwayo yeye  akiuinua Ufalme juu ya
 mahusiano na viungo vya mwili na damu alitangaza kuwa wenye heri wale wanaolisikia na kulitunza Neno la Mungu (taz Mk 3:35; Lk 11: 27-28), kama alivyofanya Maria kwa uaminifu ( taz Lk 2: 19 na 51) , ambapo alisimama imara,kwa mpango wa Mungu; akuteswa kikatili  pamoja na Mwanawe wa pekee na alijiunganisha kwa moyo wake wa kimama na   sadaka yake. Alikubali kwa upendo sadaka aliyojitoa yule dhabihu aliyemzaa mwenyewe. Mwishowe alikabidhiwa na Yesu mwenyewe akifa msalabani kama mama yake kwa mwanafunzi kwa maneno haya, “Mama, tazama mwanao”  (taz Yn  19: 26-27)
Maria baada ya kupaa kwake Bwana.
Kwa kuwa ilimpendeza Mungu sakramenti ya wokovu wa wanadamu isidhihirishwe kitukufu kabla ya kumimina Roho aliyeahidiwa na Kristo, tunawaona Mitume  kabla ya siku ya Pentekoste “wakidumu kwa moyo mmoja kaktka kusali, pamoja nao wanawake na Maria, mama yake Yesu, na ndugu zake” (Mdo 1: 14). Hata Maria aliomba kwa sala zake paji la Roho ambaye  alimfunika tayari kama kivuli siku ya kutangazwa kwake.
Mwishowe Bikira asiye na doa alikingiwa na kila doa la dhambi ya asili, (183). Akishamaliza mwendo wa maisha yake duniani, aliinuliwa katika utukufu wa mbinguni pamoja na mwili [wake] na pamoja na roho [yake] (184) akatukuzwa na Bwana kama Malkia   wa ulimwengu, ili afananishwe kikamilifu na Mwanawe aliye Bwana wa mabwana (taz. Ufu 19: 16) na mshindi wa dhambi na mauti(185).



0 comments:

Post a Comment

RICHARD MATANDA TESHA

 
Support : Richie | Bikira Maria | Elimu Endelevu
Copyright © 2013. BIKIRA MARIA - All Rights Reserved
Template Created by Mwariko Published by Mwariko team
Proudly powered by Jicho la Habari